Kocha wa Yanga Lwandamina kurudi Nchini Leo

Kocha wa Yanga, George Lwandamina anatarajia kurejea nchini leo, tayari kuanza kazi.

Lwandamina alilazimika kusafiri kwenda kwao Zambia baada ya kupata msiba wa kufiwa na baba yake mzazi.

Pamoja na msiba huo mkubwa kwake, Lwandamina aliamua kurejea haraka ili kupambana kuhakikisha kikosi chake kinafanya vizuri.

Kocha huyo mtaratibu anatarajia kurejea leo jioni na kesho ataendelea na kazi ya kukinoa kikosi chake.

Post a Comment

Previous Post Next Post