Jafo na Dkt Kigwangalla Watoa Neno Baada ya Kuapishwa

Jafo na Dkt Kigwangalla Watoa Neno Baada ya Kuapishwa


Aliyekuwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, Seleman Jafo baada ya kuteuliwa na kuapishwa kuwa Waziri wa wizara hiyo amewaahidi Watanzania kuwa wategemee utendaji mzuri wa kazi kutoka kwake huku akiwaomba watumishi wote umma kufanya kazi kwa spidi.

Wakizungumza Ikulu jijini Dar es salaam mara baada ya kuapishwa, Mhe Jafo amesema lengo lake ni kuisukuma nchi ifikie malengo yanayotarajiwa huku Dkt Kigwangalla akisema Mh. Rais ameonyesha imani kubwa sana na uwezo wake.

“Kikubwa zaidi niwaahidi Watanzani wategemee utendaji mzuri wa kazi, lakini niombe sana watumishi wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lazima wajipange kufanya kazi kwa bidii , Wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya, Wakurugenzi naomba waongeze spidi na Wakurugenzi waongeze spidi lakini watumishi wote waongeze spidi lengo ni tuisukume nchi yetu ifike katika malengo tunayoyatarijia

Hata hivyo Mhe. Jafo alipoulizwa kuwa ikiwa ni miongoni mwa Waziri walipandishwa yeye anafikiri ni kwanini kapandishwa na kuwa Waziri kamili? Akijibu “Ni mipango ya mwenyezi Mungu jambo la kwanza, la pili ni imani ya Mheshimiwa Rais kwangu, tatu ni utendaji wa kazi kwasababu ni lazima popote utakapo niweka ni lazima nifanye kazi kwasababu nina dhamana ya Watanzania naamini popote Mungu ananiona.”

Kwa upande wake aliyekuwa Naibu Waziri wa Afya ambaye kwasasa ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamisi Kigwangalla amesema kuwa “nimefarijika sana pia nimepewa imani kubwa na Mhe. Rais, nimepewa Wizara nyeti ni wizara ambayo inachangia asilimia 17.2 ya pato la taifa ni wizara nyeti sana, na mimi kupewa jukumu hili maana yake mhe. Rais ameonyesha imani kubwa sana na uwezo wangu lakini pia na uzalendo nilionao naomba niwaambie Watanzania na Mhe. Rais Kuwa sitawaangusha

Post a Comment

Previous Post Next Post