Mzee wa Upako Anena Mazito Kuhusu Waliompiga Risasi Mh. Tundu Lissu

Kwanza naanza kwa kusema nampa pole ndugu yangu, mTanzania mwenzangu Tundu lissu kwa majanga yaliyo mpata, mimi ni mkristo miongoni mwa mambo ambayo Yesu alisema na ni kauli yake ya mwisho ni Duniani mnayo dhiki alikuwa anamaanisha matukio kama haya kwamba kuna watu watanyimwa haki ya kuishi kwa sababu ya misimamo yao, na utu wao utapuuzwa kwa sababu ya misimamo yao, wataonewa kwa sababu ya mitazamo yao, hii ni Dunia matukio kama haya hayajaanza leo na wakati wote watekelezaji wa matukio kama haya wanaishia pabaya wakati utawahukumu. Ninacho muombea ndugu yangu apone haraka na Mungu amsaidie. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika

Post a Comment

Previous Post Next Post